Monday, 21 March 2016

IJUE RORYA


Wilaya ya Rorya

Rorya ni wilaya mpya katika mkoa wa Mara. Hadi 2006 ilikuwa sehemu ya magharibi ya wilaya ya Tarime. Mnamo mwaka 2007 iligawanywa kuwa wilaya. Makao Makuu ya Wilaya ya Rorya ni Ingri Juu huku mji mkubwa katika wilaya hii ni Shirati.
Wakazi walio wengi wa wilaya ya Rorya ni Wajaluo. Wakazi wengine wa eneo hili ni Wakurya, Wakine, Wasimbiti na Wasuba
Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, wilaya hii ilikuwa na wakazi wapatao 265,241 waishio humo.

Jogorafia ya Rorya

Rorya ipo Kaskazini mwa Tanzania ipo kati ya latitudo 1°00" – 1°45" kusini mwa mstari wa Ikweta na longitudo 33° 30" – 35° 0"  upande wa mashariki ya mstari wa Meridian. Eneo la wilaya ya Rorya liko kati ya ziwa Viktoria Nyanza upande wa magharibi na Tarime upandwe wa mashariki. Upande wa kaskazini inapakana na Nchi ya Kenya na upande wa kusini wilaya ya Musoma.
Wilaya hii inakadiriwa kuwa na altitudo 800mm-1200mm kutoka usawa wa bahari na jotoridi la eneo hili pia inakadiriwa kuwa ni kati ya 21-29 digrii sentigredi. Wastani wa mvua kwa mwaka inakadiriwa kuwa kati ya 700mm hadi 1200mm.


Majimbo ya uchaguzi, Tarafa na Kata
Mfumo wa Tanzania wa uchaguzi imegawa nchi katika majimbo mbalimbali ya uchaguzi. Tangu mwaka uchaguzi wa mwaka 1995 wilaya ya Rorya ina jimbo moja ya uchaguzi (Jimbo la Rorya). AidhaWilaya ya rorya ina Tarafa nne nazo ni;
1.   Girango,
2.   Nyancha,
3.   Luo-Imbo
4.   Suba
5.   Rabuor

Vilevile wilaya hii hadi kufikia mwaka 2012 ilikuwa na kata 21 nazo ni; (jumla ya wakazi mbele ya kata)

1.    Bukura - 15,228

2.   Bukwe - 9,920

3.   Goribe - 9,915

4.   Ikoma - 10,397

5.   Kigunga - 13,824

6.   Kirogo - 7,250

7.   Kisumwa - 12,447

8.   Kitembe - 9,845

9.   Komuge - 13,651

10. Koryo - 7,652

11. Kyang'ombe- 18,438

12.                Mirare - 12,416

13.                Mkoma - 17,132

14.                Nyahongo - 18,454

15.                Nyamagaro - 17,006

16.                Nyamtinga - 11,203

17.                Nyamunga - 13,161

18.                Nyathorogo- 14,809

19.                Rabour - 11,259

20.                Roche - 8,728

21.                Tai - 12,506

Uchumi

Uchumi wa Rorya ina shikiliwa na kilimo ambapo inakadiriwa takribani asilimia 89 ya wakazi wa Wilaya ya Rorya wanategemea kilimo. Eneo la wilaya ya hii ina ukubwa wa heraki 291,375 inayofaa kwa kilimo lakini ni hekari  130,481 pekee ndio inayolimwa mpaka sasa. Vilevile eneo lenye ubwa wa kilometa za mraba takriban 17350 inafaa kwa kilimo cha umwagiliaji kalini ni kilometa za mraba 1,039 pekee ndio kilimo cha umwagiliaji inafanyika. Kilimo katika wilaya ya Rorya kwa kiasi kikubwa inategemea jembe la mkono pamoja na ya kukokota na Ng’ombe. Hii hupelekea shuguli ya kilimo kuwa na tija ndogo. Aidha kilimo cha kisasa kinafanyika lakini na watu wachache. Mazao yanayolimwa katika wilaya hii ni pamoja na Mihogo, Mahindi, Viazi vitamu, Mtama, maharage, mbogamboga na matunda kwa kiasi kidogo. Shughuli zingine za kiuchumi katika wilaya hii ni pamoja na yafuatayo;

Ufugaji

Zaidi ya 70% ya wakazi wa Rorya hujihusisha na ufugaji (Ng’ombe, mbuzi, kondoo, kuku n.k). Ufugaji husaidia wakazi wa Rorya kwa kuwapatia Chakula (Nyama, maziwa, mayai n.k) pamoja na Kipato. Vile vile Mifugo hususan Ng’ombe na punda ni nyenzo inayotumika na wakazi hawa kwa ajili ya kilimo. Asilimia kubwa ya ufugaji katika eneo hili ni ufugaji wa asili jambo inayopelekea kuwa shughuli yenye tija ndogo kwa wakazi hawa.

Viwanda

Wilaya ya Rorya viwanda vidogovidogo ikiwemo Kiwanda  cha kutegeneza Sabuni, Kiwanda cha kuchakata Ngozi pamoja na kiwanda cha Maziwa. Kwa kiasi fulani uwepo wa viwanda hivi vimesaidia kutoa ajira kwa wakazi wa eneo hili lakini bado havijawa na tija kubwa kwa wakazi hawa.

Biashara

Vilevile wakazi wa Rorya hujihusisha na na biashara mbalimbali kuanzia kubwa, kati pamoja na biashara ndogondogo. Biashara inayofanyika ni pamoja na biashara ya mazao na vyakula vya aina mbalimbali ikiwemo samaki, dagaa, mbogamboga na matunda n.k. Vituo maarufu vya biashara katika wilaya hii ni pamoja na, Shirati, Utegi, Ochuna, Randa na Mthana. 

Madini

Mdini ni rasilimali nyingine inayopatikana katika eneo hili japo uchimbaji mkubwa bado haijaanza lakini kuna uchimbaji mdogomdogo inaendelea katika maeneo mbalimbali. Japo bado hakuna takwimu juu ya hali ya uchimbaji na kipato itokanayo na madini katika eneo hili lakini inasaidia kuwapatia wakazi wa eneo hili kipato. Vilevile katika eneo hili kuna uchimbaji wa mawe, kokoto na michanga kwa jili ya ujenzi.

Uvuvi

Wilaya ya Rorya ina eneo inayofaa kwa uvuvi lenye ukubwa wa kilometa za mraba 7,252 kandokando ya ziwa Viktoria ambapo jumla ya vijiji 23 vimezunguka eneo hili. Wanavijiji hawa hutegemea sana uvuvi katika kuendesha maisha yao ikiwemo kipato na chakula. Aina ya samaki inayovuliwa ni pamoja na Sangara (Mbuta-Kijaluo), Sato (Ngege-Kijaluo), Dagaa (Omena-Kijaluo).

Ufugaji wa Nyuki

Hii ni shughuli changa katika eneo hili. Haijanea miongoni nmwa wakazi wa Rorya kama shughuli ya kuingiza kipato. Ufugaji nyuki inafanyika kwa njia za asili jambo inayopelekea kuwa na manufaa madogo kwa wakazi wa eneo hili. Kuna takriban Vikundi 10  vya wajasiriamali katika vijiji mbalimbali wanaojihusisha na shughuli hii. Vikundi hivi vina jumla ya mizinga 400.

Maliasili (Misitu, milima na mito)

Wilaya ya Rorya ina maliasili mbalimbali ikiwemo Misitu, milima pamoja na Mito. Misitu inachukua eneo lenye ubwa wa kilometa za mraba takriban 1,534sawa na 30% ya ukubwa wa eneo lote la Wilaya ya Rorya. Asilimia 18 ya misitu hii humilikiwa na na jamii yenyewe, asilimia 12 na watu binafsi ijulikanayo kama Ngitiri. Misitu hii hutumika na wakazi hawa kwa ajili ya ujenzi, dawa na nishati. Vilele wilaya ya Rorya ina mito miwili mikubwa, Mto Mara na Mto Mori isiyokauka mwaka mzima. Pia kuna milima mbalimbali ikiwemo Mlima Rorya.

6 comments:

  1. Rorya ni kubwa lakini kwa idadi ya vituo maarufu kwa ajili ya biashara does not make sense. Hii inatakiwa iangaliwe kwa mapana ili kukuza uchumi wa Rorya na maendeleo yake kwa ujumla.

    ReplyDelete
  2. Hivi viwanda 3 vipo hai kweli au ni historia?

    ReplyDelete
  3. Nimeona madini kumbe mchanga

    ReplyDelete
  4. Ni vema ulivyotaja viwanda lakini haviko hai inasikitisha sana

    ReplyDelete
  5. Mtoa historia ya Rorya huyu sijui katumwa kumfurahisha nani!?Viwanda!?

    ReplyDelete
  6. Nyamaguku pia Ni kituo kikubwa Cha biashara,bila kusahau mialo maarufu Kama vile kibui,ruhu na kinesi ambapo Kuna kivuko kikubwa kinachounganisha Rorya na musoma mjini.ingefaa serikali itafute muwekezaji wa kiwanda Cha maziwa kinesi maarufu Kama Farm.kwani limekuwapori linalosaidia kwa wizi wa mifugo na kufichwa humo.

    ReplyDelete